Twapanda Mapema

 


Twapanda mapema, na mchana kutwa
Mbegu za fadhili hata jioni;
Twangojea sasa siku za kuvuna:
Tutashangilia wenye mavuno.


Refrain
Wenye mavuno, wenye mavuno,
Tutashangilia wenye mavuno.
Wenye mavuno, wenye mavuno,
Tutashangilia Wenye mavuno.


Twapanda mwangani na kwenye kivuli;
Tusishindwe na baridi na pepo;
Punde itakwisha kazi yetu hapa:
Tutashangilia wenye mavuno.


Twapanda kwa Bwana mbegu kila siku,
Tujapoona taabu na huzuni;
Tuishapo shinda atatupokea:
Tutashangilia wenye mavuno.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *