Napenda Kuhubiri

 


1. Napenda kuhubiri habari ya Yesu,
Ya Bwana wa fahari na pendo zake kuu.
Huhubiri napenda kwa hali na mali;
Mwenyewe Nimeonja najua ni kweli.


Pambio
Napenda kuhubiri kisa cha Bwana Yesu,
Ya Bwana wa fahari na pendo Zake Kuu.


2. Napenda kuhubiri mambo ya ajabu
Na tukiyatafikiri yapita Dhahabu.
Kuhubiri napenda ya yaliyonifaa;
Nami sana napenda hayo kukwambia.


3. Napenda kuhubiri, hunifurahisha
Tamu yake habari haiwezi kwisha.
Napenda kuhubiri wa gizani nao;
hawana muhubiri wa kweleza chuo.


4. Kuhubiri napenda hata wajuao;
Kusikia hupenda kama wenzi wao.
Nako kwenye fahari nikiimba wimbo
Nitaimba habari ya Mwokozi huyo!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *