Mbali kule nasikia

 


Mbali kule nasikia malaika wa mbinguni,
Wakiimba wengi pia wimbo huo juu angani:


Ref
Gloria in excelsis Deo,
Gloria in excelsis Deo.


Wachunga tuambieni sababu ya nyimbo hizo?
Mwenye kuimbiwa ni nani, juu ya nani sifa hizo?


Je hamjui jambo kuu la kuzaliwa Mwokozi?
Habari ya wimbo huo ndiyo kumshukuru Mwenyezi.


Kweli, nasi twende hima, tufike kule aliko,
Tuone mtoto na mama, tuwasalimie huko.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *