Malaika kaleta noeli

 


Malaika kaleta Noeli ya kwanza,
Kwa wachunga kondoo katika makonde,
Bethlehemu wakawa walinzi wa zamu,
Wakaona usiku ajabu ya nuru


Refrain
Noeli, Noeli, Noeli, Noeli,
Yesu yu Mungu na binadamu
Noeli, Noeli, Noeli, Noeli,
Yesu yu Mungu na binadamu


Wakaona mbinguni, mwangaza wa nyota,
Ing’aayo kwa mbali na masharikini,
Wakaenda upesi, walivyoambiwa.
Bethlehemu wamwone Mwokozi horini


Mashariki watoka wafalme watatu,
Mamajusi waliotafuta mfalme,
Wafuata hii nyota waliyoiona,
Wasipate kumkosa wanayemtafuta


Kiongozi ni nyota iliyowaleta
Hata mji wa Daudi alimozaliwa
Ikakaa mara moja isiendelee
Pale pale nyumbani alimo Mwokozi


Mamajusi walipoingia nyumbani
Wakapiga magoti kwa heshima kuu
Mara hiyo walipozifungua hazina
Manemane, uvumba, dhahabu, watoa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *