Juu ya mlima uliwekwa mti

 


Juu ya mlima uliwekwa mti,
Uliodharauliwa. Msalaba huo
Naupenda sana, Hapo Yesu ‘katufilia.


Ref
Naupenda msalaba huu,
Nitashinda kwa nguvu zake.
Naupenda msalaba huu,
Taji nitapewa huko juu.


Msalaba huo naupenda sana, Wengine
Waudharau, Kwani Mwana-Kondoo
Aliacha mbingu, Kutufilia msalabani.


Naona uzuri wa msalaba huu, Damu
Ilipomwagika. Hapo Bwana Yesu alisulibiwa,
Mkombozi wa wenye dhambi.


Nitanyenyekea penye msalaba, Kuyavumilia
Yote. Nitakaribishwa na Yesu mbinguni,
Kwenye utukufu milele.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *