Amini utii

 


Namwandama Bwana kwa alilonena,
Njia yangu huning’azia;
Nikimridhisha atanidumisha
Taamini nitii pia.


Ref
Amini utii, njia pweke ni hii
Ya furaha kwa Yesu: amini ukatii


Giza sina kwangu wala hata wingu,
Yeye mara huviondoa,
Woga, wasiwasi, sononeko, basi.
Huamini nitii pia.


Masumbuko yote, sikitiko lote;
Kwa mapenzi hunilipia,
Baa, dhara, dhiki, vivyo hubariki,
Taamini nitii pia.


Mimi sitajua raha sawasawa
Ila yote Yesu kumpa;
Napata fadhili na radhi kamili,
Taamini nitii pia.


Nitamfurahisha na kumtumaini,
Majumbani na njia-njia;
Agizo natenda, nikitumwa hwenda,
Huamini nitii pia

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *