Yesu kwetu ni rafiki

 


Yesu kwetu ni Rafiki,
Huambiwa haja pia;
Tukiomba kwa Babaye
Maombi asikia;
Lakini twajikosesha,
Twajitweka vibaya;
Kwamba tulimwomba Mungu
Dua angesikia.


Una dhiki na maonjo?
Una mashaka pia?
Haifai kufa moyo,
Dua atasikia.
Hakuna mwingine mwema
Wakutuhurumia;
Atujua tu dhaifu;
Maombi asikia.


Je, hunayo hata nguvu,
Huwezi kwendelea,
Ujapodharauliwa
Ujaporushwa pia.
Watu wangekudharau
Wapendao dunia,
Hukwambata mikononi,
Dua atasikia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *