Wimbi La Damu

 


Wimbi la damu ya Yesu Linatutakasa;
Aliumia kusudi Tupate uzima.


Chorus
Wimbi la damu naona, Naingia, natakaswa!
Bwana asifiwe sana, Hutakasa, hutakasa.


Damu inasema kwangu, Nasikia mvuto;
Inasema, moyo wangu Hutakaswa nayo.


Naondoka kutembea Kwa nuru ya mbingu;
Mavazi yamesafishwa; Moyoni ni Yesu.


Neema ni ya ajabu, Kutakaswa ndani!
Na kuwa naye Yesu tu, Aliye Mwokozi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *