Nilitembea mbali katika dhambi

 


Nilitembea mbali katika dhambini,
Nikapoteza hali nikashuka chini;
Kwake Mwokozi Bwana, nikamlilia
Akanishika sana kuokoa.


Ref
Na upendo, Na upendo,
Nimeinuliwa sana na upendo;
Na upendo, Na upendo,
Nimeinuliwa sana na upendo;


Moyo wangu nampa, nitamshika pia
Nitakaa na Yesu, sifa kumwimbia:
Upendo wa hakika wastahili sifa,
Na uaminifu ni wake pia.


Mliomo shidani, tazameni Bwana,
Atawaponya kweli, kutoka mashaka;
Atawasimamisha na upendo wake,
Awe Mwokozi kwa wokovu wake.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *