Ni Tabibu wa Karibu

 


1. Ni tabibu wa karibu, Tabibu wa ajabu,
Na rehema za daima, Ni dawa yake njema.


Ref
Imbeni, malaika, sifa za Yesu Bwana
Pweke limetukuka, Jina lake Yesu.


2. Hatufai kuwa hai, wala atutumai,
Ila yeye kweli ndiye Atupumzishae.


3. Dhambi pia na hatia, Ametuchukulia
Twenendeni kwa Amani, Hata kwake Mbinguni.


4. Huliona tamu jina, La yesu kristo bwana,
Yuna sifa mwenye kufa, Asishindwe na kufa.


5. Kila mume asimame Sifa zake zivume;
Wanawake na washike, Kusifu jina lake.


6. Na vijana vyote tena, Vimpendavyo sana;
Vije kwake viwe vyake, Kwa utumishi wake.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *