Ndiyo dhamana

 


Ndiyo dhamana, Yesu wangu,
Hunipa furaha za mbingu,
Mrithi wa wokovu wake,
Nimezawa kwa roho wake.


Ref
Habari njema, raha yangu,
Yesu ndiye Mwokozi wangu,
Habari njema, raha yangu,
Yesu ndiye Mwokozi wangu.


Kumsalimu moyo wangu,
Mara namwona raha yangu,
Aniletea malaika,
Wanilinda, taokoka.


Sina kinyume; nashukuru,
Mchana kutwa huja kwangu,
Usiku kucha kuna nuru,
Mwokozi wangu; ndimi nuru.


Hali na mali, anitwaa!
Mara namwona anifaa,
Nami nangonja kwa subira,
Akiniita nije mara.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *