Nataka kusimama

 


Nataka kusimama, chini ya msalaba.
Kama kivuli cha mwamba, wakati wa mchana.
Kama ni maji nyikani, kambi safarini.
Na hapa nitapumzika, kwani jua kali.


Mahali pema sana, chini ya msalaba.
Kwani hapo ninaona, upendo wa Yesu.
Yakobo alivyoona, ndotoni zamani.
Mti Yesu aliowambwa, ni ngazi kwa Mungu.


Juu ya msalaba huo, Yesu alikufa.
Alikufa tuokoke, tuliopotea.
Ninastaajabu kabisa, Ni mambo mawili;
Kwake Yesu ni upendo, kwangu mimi kosa!


Wataka kuonana, na Yesu mbinguni,
Yakupasa kukaa kwanza, chini ya mti huo.
Ni kweli siku chache tu, mateso na shaka.
Halafu pasipo mwisho, furaha kwa Bwana!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *