Nasifu Shani Ya Mungu

 


Nasifu shani ya Mungu, mweneza bahari,
Muumba pia wa mbingu, jua, nyota, mwezi,
Ni tukufu yako shani, mtengeza mambo,
Ya nyakati na zamani, yasiyo na mwisho.


Kadiri ya nionayo, ya kusifu Mungu;
Nchi niikanyagayo, na hayo mawingu;
Hakuna hata unyasi, usiokukuza;
Na upepo wavumisha, au kutuliza.


Nami kwa mkoni wako, naongozwa sawa,
Ni pato nikusifupo, kukwomba ni dawa;
Umenizingira nyuma, na mbele baraka;
Maarifa ya ajabu! Yanishinda mimi!

https://youtu.be/bd5M9ksUHns

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *