Naendea msalaba

 


1. Naendea msalaba, Ni mnyonge, mpofu,
Yapitayo naacha nipe msalaba tu.


Ref
Nakutumaini tu, wee Mwana wa Mungu;
Nainamia kwako; Niponye sasa, Bwana.


2. Nakulilia sana: Nalemewa na dhambi;
Pole Yesu asema: “Nitazifuta zote.”


3. Natoa vyote kwako, nafasi nazo nguvu,
Roho yangu na mwili viwe vyako milele.


4. Kwa damu yake sasa amenivuta sana,
Upendo hubidisha, nimtafute Mwokozi.


5.Yesu yuaja tena! Nimepevuka kwake,
Kila chembe kamili; Msifuni yeye mponya!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *