Lo Ajabu Kupata Uzima

 


Lo! Ajabu kupata Uzima, katika damu ya Mwokozi wangu!
Alinifilia pendoni, Mimi niliyemsulubisha!
Upendo huu wa kushangaza kabisa Wewe Kristo wangu kunifilia pendoni
Upendo huu nashangaa Kristo wangu kunifilia


wangu alitoa damu Siwezi kuelewa neno hili,
Viumbe vyote vya mbinguni Navyo haviwezi kufahamu
Najua tu ni kwa rehema zake Mungu Malaika wote wamsujudu Mungu
Ni rehema tumwabudu, Tumwamini ndiye mwokozi


Aliondoka kule mbinguni Kwa nyumba yake Mungu Baba yake
Na utukufu aliacha Afe kwa ajili ya waovu
Rehema zake ni nyingi na ukarimu Kwani Mungu wangu aliniokoa mimi
Sistahili neema yake, Lakini aliniokoa


Roho yangu ilifungwa sana Dhambi na giza vilinilemea
Ukaniangaza rohoni, Gereza yangu ikaang’aa mno
Ikafunguka minyororo yangu yote Nikaondoka nikaanza kukufuata
Siku ile nitapata Uhuru kweli kwako Mungu


Hukumuni mimi simo sasa Mimi ni wake Yesu ndiye wangu
Yeye ni kichwa changu kweli Na amenivika haki yake
Mimi hodari sasa kwa kiti cha Enzi Napewa taji ya milele katika Yesu
Sina hofu kusogea Katika Bwana wangu Kristo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *