Kaa Nami


1. Kaa nami ni usiku tena; usiniache gizani, Bwana,
Msaada wako haukomi; Nili peke yangu, kaa nami.


2. Siku zetu hazikawi kwisha; Sioni la kunifurahisha;
Hakuna ambacho hakikomi, Usiye na mwisho kaa nami.


3. Nina haja nawe kila saa; sina mwingine wa kunifaa
Mimi nitaongozwa na nani ila wewe? Bwana kaa nami.


4. Sichi neno uwapo karibu; Nipatalo lote, si taabu;
Kifo na kaburi haviniumi; Nitashinda kwako, kaa nami.


5. Nilalapo nikuone wewe; Gizani mote nimulikiwe;
Nuru za mbinguni hazikomi, siku zangu zote; kaa nami.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *