Jina Langu Limeandikwa Je

 


1. Sitafuti mali, wala utajiri;
Nataka kwa yakini nipate Mwokozi.
Chuoni mwa Ufalme, niambie Yesu,
Jina langu yakini limeandikwa, je?


Chorus:
Limeandikwa, je? Jina langu huko?
Kitabuni mbinguni, limeandikwa je?


2. Dhambi zangu ni nyingi, ni kama mchanga,
Lakini damu yako, Mwokozi, yatosha;
Kwani umeahidi; zijapo nyekundu
Zitakuwa nyeupe ilivyo theluji.


3. Mji mzuri sana, wa majumba makuu,
Walipo malaika, mji bila ovu;
Wakaapo walio na mavazi safi,
Limeandikwa sasa, jina langu huko?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *